MBOWE NA WENZAKE WAACHIWA HURU.

 


Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani Muda huu

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Ikupendeze naitwa Robert Kidando Wakili wa Serikali Mwandamizi nipo na

Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Ignasi Mwinuka
Mawakili Wa Serikali Waandamizi Tulimanywa Majige
Wakili wa Serikali

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na

Paul Kisabo
Sisty Aloyce
Gaston Garubindi
Iddi Msawanga
Evaresta Kisanga
Maria Mushi
Nashon Nkungu
John Mallya
Jeremiah Mtobesya
Fredrick Kihwelo
Dickson Matata Ni hayo tu mh Jaji.

Jaji: Shauri lilikuwa lina kuja kwa Utetezi, Je Mnazo habari zozote za Wateja wenu?

Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji ni kweli Kwamba Shauri lilikuwa limepangwa kwa ajili ya Utetezi Kwa Upande wangu tulifanya Maandalizi Mazuri Mimi John Malya, Dickson Matata, Fredrick Kihwelo na

Kibatala: wengine Juzi na Jana tulikuwa Ukonga na Segerea. Tulionana nao wakiwa na Bashasha kabisa, Kwamba Leo tunaendelea na Utetezi Lakini Leo Asubuhi tumepata Taarifa Kutoka Kwa Askari Magereza Kwamba Mbowe amepata Matatizo ya Ki Afya. Kwa hiyo hatuwezi Kuendelea,

Hivyo, Tunaweza Kupanga Kuendelea Jumatatu

Jaji: Jumatatu itakuwa Tarehe ngapi

Wakili Peter Kibatala: Tarehe 07 March 2022

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Utetezi, na tumewasikia Wenzetu Maombi Waliyo Wasilisha Sasa tusingependa Kujibu Hoja hiyo, Kwa sababu na sisi tuna Maombi Mengine Kwa hiyo Kujibu Hoja hiyo haitokuwa na Maana sana

Mheshimiwa Jaji tunaomba Moja la Kufanya Mbele ya Mahakama yako Na Ombi hili Mheshimiwa Jaji ni kwamba Mkurugenzi Wa Mashitaka (DPP) kwa niaba ya Jamhuri anaomba Kuwasilisha Taarifa ya Kutokuwa na Nia na Kuendelea na Shauri hili

Na Taarifa hiyo tunaitoa Chini ya Kifungu cha 91(1) kwa Sheria ya Mwenendo Wa Makosa ya Jinai

Jeremiah Mtobesya: Tumesikia Taarifa ya Notes hiyo kutoka kwa Mkurugenzi Wa Mashtaka, na Kwa Bahati Mbaya hatuwezi Kusema lolote zaidi ya Kusema tunaichia Mahakama, sababu Kifungu Kinatoa Maelezo Yote Kwamba Baada ya Kusema hivyo tunaichia Mahakama dhidi ya Amri zake za Mwisho

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Taarifa Hii tunaiwasilisha kwa Njia ya Maandishi, Kwa Maombi hayo ya Kifungu cha 91(1) tunaomba Kuondoa Mashitaka Yote dhidi ya Washitakiwa Wote Sababu zote zipo katika Noel Prosecui ambayo tumeiwasilisha

Wakili wa Serikali Robert Kidando: anapeleka Nyaraka Mbele ya Karani wa Jaji, na Karani anampatia Jaji

Jaji: Je umezungumza kwa niaba ya Defense Wote..?

Jeremiah Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba kila Mmoja aseme

John Malya: Mheshimiwa Jaji notes iliyotolewa inayushuka Mikono wote, pamoja na Kujiandaa kwa ajili ya Kujitetea, Mikono yetu imefungwa na hatuwezi Kusema lolote, Tulitaka sana Warudishe Gharama zetu na Mengine lakini wacha Tusubiri Maamuzi ya Mahakama

Fredrick Kihwelo: Kwa niaba ya Mshtakiwa wa tatu Tumesikia Taarifa iliyotolewa, Tunaichia Mahakama iweze Kutoa Amri

Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Na sisi tunaichia Mahakama, Sheria inajielezea wazi.. Mahakama ipo Kimya Kidogo na Jaji Bado anaandika

Kule Nje ni Kelele za Shangwe na Fifijo watu Wanaimba, Imebidi Mahakama Kufunga Vioo Vya Madirisha ili Kuzuia Kelele Kuingia Mahakamani, Wewe furaha yako ni Kiwango gani? Onyesha emoji ya furaha hapa Chini.. Au picha yako ukiwa na furaha kubwa.

Jaji: Baada ya Mahakama Kusikiliza Hoja iliyoletwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali Kwamba Mkurugenzi wa Mashtaka hana nia ya Kuendelea na Kesi, na Upande wa Pili wakaridhia

Mahakama inasema Shauri hili lililo kuwa linawakabili Washitakiwa Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa nakiondosha Mahakamani na Washitakiwa Wanaachiwa huru bila Masharti, sababu Kuna Vielelezo vililetwa Mahakamani, naandaa Amri ya Kuviachia

Jaji: Na hivyo naelekeza Mkuu wa Magereza Kuwaachiwa Mara Moja, Leo na si Vinginevyo Natoa Amri Jaji anatoka Mahakamani Mahakama inaridima Kwa Shangwe.
Freeman Aikael Mbowe na wenzake watatu, wameaachiwa huru leo, na Mahakama kuu Divisheni ya makosa ya uhujumu uchumi na Rushwa, Baada ya DPP Kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na shauri hilo, leo 4.3.2022. Hivyo, Freeman Aikaeli Mbowe


Comments

News