BUSARA ZA ROMAN,MO NA GSM WAJIFUNZEHAPA JUU YA MUSTAKABALI MPANA WA VIGOGO WA KARIAKOO

 

Bilionea ambaye ni Mmiliki wa Club ya

Chelsea ya England Roman Abramovich

amethibitisha kuwa anataka kuiuza club hiyo

ambapo anafanya hivi kwa maslahi mapana

ya Club, Wadhamini na Wafanyakazi wa Club.

Ningependa kutoa taarifa kuhusiana na

tetesi zinazoendelea kwenye vyombo vya

habari kuhusiana na umiliki wangu Chelsea,

siku zote nimekuwa nikifanya maamuzi kwa

sababu ya maslahi ya club, kwa hali

inavyoendelea sasa nimeamua kuiuza club"

Roman Abromavich.

--

Roman aliinunua club hiyo 2003 kwa pound

milioni 140 (Tsh Bilioni 433) na sasa

ameamua kuiuza baada ya vita ya Ukraine

kuisababishia Russia na Wawekezaji wake

kuwekewa vikwazo au biashara zao

kusitishwa sehemu mbalimbali.

Kwa mujibu wa Forbes Chelsea sasa ina

thamani ya pound Bilioni 2.4 (Tsh Trilioni

7.4).

Roman katika taarifa iliyotolewa na Chelsea

anasema atauza club hiyo na pesa zote

alizouza zitaenda katika mfuko maalum wa

kusaidia Waathirika wa vita nchini Ukraine na

wala hana lengo la kujipatia faida.


Comments

News