Semina ya TAKUSKA WILAYA YA RUFIJI MUWAKILISHI WA DC AFISA ELIMU TAMADUNI ASIMAMIA SHOW VYEMA


 

Leo Februari 23. 2022 imetaranyika semina yamwongozo wa kuzuia na

kupambana na Rushwa kwa Vijana wa Skauti

mashuleni na Vyuoni katika Ukumbi wa chuo

Cha maendeleo ya WaNananchi (FDC) IkwiririWilayani Rufiji.



Mafunzo hayo yalihudhuriwa na Kamanda wa

TAKUKURU Wilaya, Kamanda wa TAKUKURU






Ikwiriri, Maafisa toka idara ya Elimu Msingi

na Sekondari, Maafisa elimu kata, Wakuu wa

Shule, Walimu wakuu pamoja na Kamati

tendaji ya Skauti ngazi ya Wilaya.

Awali akisoma ujumbe kwa niaba ya Mkuu

wa Wilaya ya Rufiji, Afisa Elimu Taaluma

Wilaya ya Rufiji Tunsume Mwakipesile

alisema Utekelezaji wa Mwong0zo huo

utawawezesha Vijana wa skauti kuwa

wawajibikaji, wazalendo na kujenga Jamii

itakayoichukia Rushwa.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Elimu

ambaye pia ni Afisa Elimu Vifaa na Takwimu

Sekondari Geoffrey Mwakagali amewataka

Walimu Wakuu na Wakuu wa shule

kuhakikisha wanaanzisha na kuhuisha klabu

za wapinga Rushwa mashuleni na kuwataka

kuzungumza suala la mapambano dhidi ya

Rushwa Kama ajenda katika vikao vya

wazazi.

Kwa upande wake Kamishna wa skauti

Wilaya ya Rufiji Latifa Lukwaro ametoa shukrani kwa Mkuu wa Wilayà ya Rufiji

ambaye pia ni Mlezi wa Chama Cha Skauti

Wilaya, pamoja na Mkurugenzi mtendaji wa

Halmashauri kupítia Maafisa elimu Msingi na

Sekondari kwa kutoa ushirikiano na

kuwezesha Shughuli za Vijana wa skauti

shuleni.

Emmanuel Kapandila

(Cc) Rufiji Dc.





Comments

News