MADAWATI 576 KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU

 

Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Meja Edward

Gowele amekabidhi madawati 100 kwa

Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Kilimani na

kumtaka kuyatunza madawati hayo ili

yaendelee kutoa ari ya usomaji kwa

wanafunzi

Awali, akitoa taarifa fupi ya uboreshaji wa

miundombinu ya shule za msingi kwa niaba

ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri,

Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Rufiji Edward

Buganga amesema, Halmashauri ya Wilaya

ya Rufiji Imetoa jumla ya shilingi Milioni 34.6

mapato ya ndani kutengeneza madawati 576

ambapo kati ya madawati hayo madawati

100 yamekamilika na mengine yakiwa katika

hatua ya ukamilishaji huku tenda zikiwa

zimetolewa kwa vikundi mbalimbali vya

mafundi wilayani humo.

Aidha Mhe. Gowele ametoa shukrani kwa

mdau wa elimu ambaye amejitolea usafiri

kusafirisha madawati hayo toka ikwiriri hadi

shuleni na kutoa wito kwa wadau wengine

wa maendeleo kuendelea kushirikiana na

jamii za wanarufiji kuchangia katika shughu

za maendeleo.


"Tunamshukuru sana mdau wa maendeleo
toka kilimani kwa kujitoa kusafirisha
madawati haya 100 bure hadi shuleni. Na
nitoe wito kwa wadau wengine kuiga mfano
huu kwa kushirikiana na wananchi kuchangia
katika shughuli za maendeleo" alisema
Gowele
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa sule
hiyo ameishukuru serikali kwa namna
ambavyo inaendelea kuboresha
miundombinu ya elimu na kueleza kuwa
madawati hayo yanaenda kupunguza kwa
kiasi kikubwa changamoto ya upungufu wa
madawati.
Shule ya msingi kilimani inajumla ya
wanafunzi 1554 ambapo awali tulikuwa na
upungufu wa madawati 172 hivyo madawati
haya 100 yatapunguza changamoto ya
madawati kiasi kikubwa" alisema
SOURCE RUFIJI DC.

Comments

News