Kituo cha Huduma za Pamoja Mkoani Pwani chamkosha Mhe. Bashungwa Awataka Wakuu wa Mikoa kuiga mfano wa Pwani.

 

OR-TAMISEMI

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais ofisi,

TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa

amefurahishwa na Kituo cha Huduma za

Pamoja ( One Stop Center) kilichoanzishwa

kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

kwa ajili ya kutoa huduma za haraka kwa

Wananchi wa Mkoa huo.


Akizungumza akiwa ziarani Mkoani Pwani

Mhe. Bashungwa amesema uwepo Huduma

muhimu sehemu moja inamrahisishia

mwananchi kutohangaika kuzunguka mji

mzima kutafuta Ofisi mbalimbali za kutatua

shida zake.


Katika kituo hiki tunaona huduma

mbalimbali zinapatikana katika eneo moja

hapa tunawaona TRA, Uhamiaji, DAWASA,

Magereza,TANROAD,TARURA, NEMC,

TANESCO na wengine wengi sasa

mwananchi wetu wanaweza kunaliza shida

zao sehemu moja na sio ile mtu anafunga

safari mpaka Ofisi flani kisha unaambiwa


suala hili sio la hapa nenda Ofisi nyingine
inachosha lakini kwa hapa mahitaji mengi yawananchi yanatatuliwa sehemu moja,
alisema Bashungwa.

Sasa Niwatake Wakuu wa Mikoa yote nchini
kuiga mfano huu na kuanzisha One Stop
Center kwenye Ofisi zao ili wananchi wa
maeneo hayo waweze kupata huduma bora
kwa urahisi na sio kusumbuka kama zamani.

Kituo cha Huduma za Pamoja Mkoani Pwani
kimeanza takribani mwezi mmoja sasa na
kinajumuisha Taasisi zote Wezeshi kutoka
huduma katika eneo moja.

Comments

News